Cristiano Ronaldo amemvisha pete ya uchumba mpenzi wake wa muda mrefu, Georgina Rodriguez. Wawili hao wamekuwa kwenye mahusiano kwa miaka 9 sasa na tayari wana watoto wawili pamoja.
Georgina ameweka picha ikimuonesha akiwa amevalia pete ikiambata na caption isemayo “Yes I Do” akimaanisha amekubali kuolewa na nyota huyo wa Al Nassr ya Saudi Arabia
