Watu wengi hawapati usingizi wa kutosha katika siku za kazi zenye misongamano, lakini utafiti unaonyesha kuwa kulala zaidi mwishoni mwa wiki kunaweza kupunguza hatari ya kupata magonjwa ya moyo na hata kuzuia mshutuko wa moyo.
Tafiti zimebaini kuwa ukosefu wa usingizi mzuri siku za wiki huongeza hatari ya kupata shinikizo la damu, uvimbe mwilini na matatizo ya moyo. Hata hivyo, watu wanaoongeza usingizi wa kurejesha mwishoni mwa wiki walionekana kuwa na hatari ya chini kwa asilimia 20 ya matatizo ya moyo ikilinganishwa na wale wanaokosa usingizi muda wote.
Pamoja na hayo, usingizi wa kurejesha mwishoni mwa wiki si suluhisho kamili, kwani kupata usingizi wa kutosha na wa kudumu kila siku za wiki ndicho kinga madhubuti zaidi kwa afya ya moyo wa muda mrefu, ilhali usingizi wa mwishoni mwa wiki husaidia tu kupunguza baadhi ya madhara ya ukosefu wa usingizi.

