Katika taarifa iliyotolewa jana Oktoba 10, 2025, kwa pamoja na wabunge wa EU, Barry Andrews, Robert Biedrón, Udo Bullmann, Michael Gahler, Erik Marquardt na David McAllister, wamesema wana wasiwasi mkubwa kuhusu matukio ya utekaji na ukandamizaji dhidi ya wapinzani wa kisiasa, wakosoaji wa Serikali na waandishi wa habari nchini Tanzania.
“Tunatoa wito kwa mamlaka husika kuhakikisha usalama wa Polepole na kuchukua hatua madhubuti kumaliza mwenendo wa vitisho na ukiukwaji wa haki za binadamu,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.
