Site icon Bongo Plus

Trump Anadai Kuwa Rais Wa Urusi Putin Anachezea Moto

Rais wa Marekani Donald Trump alisema ameiokoa Urusi kutokana na “mambo mengi mabaya sana.”

“Vladimir Putin hatambui kwamba ikiwa sio mimi, mambo mengi mabaya yangekuwa yametokea Urusi kufikia sasa, aliandika kwenye mtandao wa kijamii wa Truth Social, bila kutoa maelezo ya kina “Anacheza na moto!” – Trump aliongeza.

Siku moja kabla, baada ya siku tatu za mashambulizi makubwa ya makombora ya Urusi na ndege zisizo na rubani katīka miji ya Ukraine na kuua raia 12, rais wa Marekani alimkosoa vikali Putin, ambaye Trump alisema “amekuwa mwendawazimu” kwa kuua watu “kiholela”

Jarida la Wall Street Journal limegundua kuwa Trump anafikiria kuweka vikwazo vipya dhidi ya Urusi, lkulu ya Urusi ilisema Trump “anaendeshwa na hisia.”

Exit mobile version