Peter Okoye Wa Psquare Atoa Ushahidi Kesi Ya Ndugu Yake.

Peter Okoye Wa Psquare Atoa Ushahidi Kesi ya Ndugu Yake.

Tume ya Kupambana na Ufisadi na Uhalifu wa Kifedha (EFCC), Jumatatu, Aprili 14
ilimuwasilisha Peter Obumuneme Okoye kama shahidi wake wa kwanza dhidi ya Jude Chigozie Okoye, kaka yake mkubwa na Meneja wa zamani wa Paul na Peter Okoye,
maarufu kama PSquare, mbele ya Jaji A. Owoeye wa Mahakama Kuu ya Shirikisho iliyoko lkoyi, Lagos.

Wakati wa kuendelea kwa kesi hiyo siku ya Jumatatu, Aprili 14, Peter alipokuwa akihojiwa na wakili wa upande wa mashtaka, Aso Larry’s Peters, alisema:
“Kundi la P-Square lilianza takriban mwaka 1997. Lakini mnamo mwaka 2017, lilivunjika. Tulikaa mbali kwa takriban miaka mitano. Lakini mwezi Novemba 2021, kundi likarudi tena Kabla Jude hajawa Meneja wetu, tulikuwa na mameneja kadhaa, wakiwemo Chioma Ugochi, aliyekuwa anatusimamia tulipokuwa shule ya sekondari na chuo
kikuu na marehemu Bayo Odusami wa Mbuntu Music aliyetusimamia kwa miaka mitano Baada ya hapo, mimi na ndugu yangu pacha tulisimamia bendi kwa miezi michache kabla ya kuamua kwamba
Jude awe meneja wetu pamoja na kampuni ya Northside Entertainment Limited.

Tuliendelea kuendesha biashara yetu, lakini tulikuwa tukipata matatizo kuhusu jinsi alivyokuwa anaendesha biashara hiyo.

Matatizo  yalikuwa hasa juu ya yeye kuwe
msimamizi pekee wa akaunti zote za benki  Ecobank, Zenith, na FCMB.

Matatizo haya yalidumu kwa miezi kadhaa. Sikuwa na ufikiaji wa akaunti hizo hadi Waziri wa sasa wa Usafiri wa Anga, BW. Festus Keyamo, SAN, aliyekuwa wakili wetu, aliposema tunahitaji mfumo wa mgawanyo.

Akiendelea kutoa ushahidi, alikumbuka tukio walipokuwa wanajenga nyumba zao huko lkoyi, na kusema: “Fedha za mradi wa ujenzi wa nyumba zilikuwa zinatoka Northwest Entertainment Ltd. Lakini walikoma kufadhili ujenzi wa nyumba yangu kwa miezi sita.

Akaunti hizo zilikuwa za kampuni, lakini Jude ndiye alikuwa msaini pekee wa akaunti zote. Wakati fulani, nilimwendea yeye na ndugu yangu pacha, Paul, kuuliza kwa nini walikoma kufadhili mradi wangu. Lakini jibu nililopata kutoka kwao lilikuwa: ‘Ukitoka P-Square, umetoka na hela pia.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button