Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Patrobas Katambi amesema kuwa ndoa ni kiini cha msingi, nguzo imara
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe.
Patrobas Katambi amesema kuwa ndoa ni kiini cha msingi, nguzo imara na kiunganishi kati ya uwepo wa Serikali na masuala yote ya amani na usalama wa taifa lololote.
Ameyasema hayo leo wakati akizungumza katika hafla ya kufunga ndoa za pamoja kwa wanandoa 130, iliyofanyika katika Ukumbi wa DYCCC Chang’ombe jijini Dar es Salaam.
Hafla hiyo, imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, dini, ndugu na jamaa wa wanandoa pamoja na wananchi waliofika kushuhudia tukio hilo.






