KATAMBI KUFUNGA MAFUNZO YA ASKARI 1000 ZIMAMOTO
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mheshimiwa Patrobas Katambi amewasili wilayani Handeni Mkoani Tanga ambapo anatarajiwa kufunga Mafunzo ya Awali,Kozi Na.6/2026 katika Chuo Jeshi la Zimamoto na Uokoaji ambapo askari 1000 wanahitimu mafunzo hayo leo,tarehe 24/6/2026.
Mafunzo hayo yanayohitimishwa leo yanajumuisha Wataalamu katika kada za Uzimaji Moto wa Kemikali,Maokozi ya Angani,nchi kavu na majini ambapo wanaume wapo 651 na wanawake 349.






