Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo (Ushirika na Umwagiliaji), Dkt. Suleiman Serera ameripoti kazini na kupokelewa na Viongozi mbalimbali wa Wizara akiwemo Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo (Ushirika na Umwagiliaji), Dkt. Suleiman Serera ameripoti kazini na kupokelewa na Viongozi mbalimbali wa Wizara akiwemo Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb), Katibu Mkuu Bw. Gerald Mweli, Naibu Katibu Mkuu (Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula), Dkt. Hussein Omar pamoja na watumishi wa Wizara leo tarehe 14 Agosti 2024, jijini Dodoma.
Dkt. Serera aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan mnamo tarehe 13 Agosti, 2024 kushika wadhifa huo.







