Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Said Mtanda Ofisini kwake Mkoani Mwanza kuhusu maandalizi ya ufunguzi wa Daraja la JP Magufuli
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Said Mtanda Ofisini kwake Mkoani Mwanza kuhusu maandalizi ya ufunguzi wa Daraja la JP Magufuli (Kigongo – Busisi) lenye urefu wa kilometa 3 na barabara za maingilio kilometa 1.66 Mkoani humo.
Daraja hilo litafunguliwa rasmi Juni 19, 2025 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.







