Balozi wa Marekani apongeza uteuzi wa Dkt. Biteko

✅️Dkt. Biteko aahidi ushirikiano na Mashirika ya Kimataifa Sekta ya Nishati.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mheshimiwa Dkt. Doto Biteko amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Marekani nchini Tanzania Dkt. Michael Battle, alipomtembelea leo, Septemba 13, 2023 katika ofisi ndogo za Wizara ya Nishati jijini Dar es Salaam.

Dkt. Battle amemtembelea Mhe. Biteko kwa lengo la kumpongeza kwa uteuzi na majukumu yake mapya ikiwa ni pamoja na kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano wa kisekta baina ya nchi hizo mbili.

Katika mazungumzo yao Mhe. Biteko ameeleza kuwa, Wizara ya Nishati itaendelea kushirikiana na wadau wa kitaifa na kimataifa katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Sekta ya Nishati ikiwemo ya uzalishaji umeme pamoja na Mradi wa kubadili Gesi Asilia kuwa katika hali ya kimiminika (LNG).

Mhe. Biteko amesema kuwa, majadiliano baina ya Serikali na wawekezaji wa Mradi wa LNG yako katika hatua nzuri na wataalamu wanaendelea kupitia vipengele vya mkataba huo ili kuhakikisha kila upande umeridhika.

Aidha amegusia kuwa upo uwezekano wa kurudia baadhi ya vipengele ili kuviboresha zaidi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button