Trump na Putin Wateta Kumaliza Vita Iran
Trump na Putin Wateta Kumaliza Vita Iran
Rais wa Marekani, Donald Trump na Rais wa Urusi, Vladmir Putin wamefanya mazungumzo kwa njia ya simu jana March 09,2026 ambapo pamoja na mambo mengine Viongozi hao wamejadiliana kuhusu kumaliza vita vinavyoendelea mashariki ya kati kati ya Marekani/Israel na Iran pamoja na vita ya Ukraine.
Trump amesema Putin ametaka kusaidia mchakato wa kumaliza mapigano kati ya Marekani, Israel na Iran lakini yeye akamshauri kuwa anaweza kuwa msaada zaidi kama atamaliza vita vya Ukraine na Urusi.
Mazungumzo hayo yamedumu kwa saa moja yakihusisha pia Viongozi wengine wa Mataifa hayo mawili na ni mazungumzo ambayo yanatajwa na Trump na Putin kuwa yalikuwa mazuri.





