Watanzania jengeni utamaduni wa kupima Afya Mara kwa Mara
TANZANIA JENGENI UTAMADUNI WA KUPIMA AFYA MARA KWA MARA
Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Dodwin Mollel ametoa wito kwa watanzania wote kuwa na utamaduni wa kupima afya zao sababu Afya ndio mtaji wa kwanza kwa kila mtu
“Mimi huwa na utaratibu wa kupima Afya yangu karibu kila mwaka, leo nimekuja tena, Taasisi ya Saratani Ocean Road kutimiza utaratibu wangu wa kufanya uchunguzi wa Afya, hususan Sarataniβ, Dkt. Mollel
Dkt. Mollel ametoa wito huo Jijini Dar Es Salaam wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya kwa wananchi na kuongea na menejimenti ya watumishi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road.