Waziri Mkuu wa Senegal Amkosoa Rais Hadharani.
Waziri Mkuu wa Senegal Amkosoa Rais Hadharani
Waziri Mkuu wa Senegal Ousmane Sonko amemkosoa hadharani Rais Bassirou Diomaye Faye, na kuashiria hali nadra ya Upinzani wa wazi ndani ya Uongozi wa juu wa nchi.
Akizungumza katika mkutano wa Chama cha Pastef, Sonko alimshutumu Rais kwa kukosa Mamlaka na kukosa kumtetea huku kukiwa na mashambulizi ya umma.
Alidai kuwa Urais haufanyi vya kutosha kuunga mkono mageuzi ya Serikali na alionyesha kufadhaika juu ya uwezo mdogo wa kutawala kwa ufanisi.
Sonko, ambaye alikuwa amemteua Faye kama mgombeaji Urais wa Chama hicho mnamo 2024 baada ya kuenguliwa kwake kisheria, sasa anaonekana kutilia shaka mienendo ya uongozi.
Waziri Mkuu Sonko ametoa wito kwa Rais Faye kusimamia majukumu yake kama Rais kwa ajili ya maendeleo ya nchi.





