Gamondi- Apigwa faini ya Tsh 2,000,000
KAMATI ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imempiga faini ya Tsh. 2,000,000 (milioni mbili) Kocha mkuu wa klabu ya Yanga, Miguel Gamondi kwa kosa la kufanya vurugu ikiwemo kuwashambulia kwa maneno makali waamuzi wa mchezo kati ya Yanga na Kagera Sugar ambapo yanga alishinda kwa goli 1-0.