MAJALIWA ATETA NA WAZIRI MKUU WA CÔTE D’IVOIRE

▪️Wakubaliana kuanzishwa kwa Jukwaa la Wafanyabiashara

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekutana na Waziri Mkuu wa Côte d’Ivoire, Robert Beugre Mambe na kujadiliana naye masuala ya kidiplomasia, kiuchumi, teknolojia, kilimo na michezo kwenye kikao kilichofanyika ofisini kwa mwenyeji wake, Boulevard Angoulvant Plateau, jijini Abidjan.

Akitoa ufafanuzi mara baada ya kikao hicho jana jioni (Jumanne, Mei 13, 2025), Waziri Mkuu Majaliwa alisema lengo la kikao chao lilikuwa kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia lakini pia kuhimiza haja ya nchi hiyo kushirikiana na Tanzania kwenye masuala mbalimbali ikiwemo utafiti na teknolojia za kisasa kwenye kilimo.

“Côte d’Ivoire ina wakazi zaidi ya milioni 31 na inaongoza kwa kilimo cha kakao, korosho na michikichi. Hawa wanalima korosho zaidi kuliko Tanzania, na sisi tunalima korosho kwenye mikoa ya Pwani na kakao kule Mbeya na maeneo mengine. Tunaweza kujifunza kwao na sisi tunaiona hii ni fursa kwetu ya kuongeza uzalishaji kwenye mazao haya.”

“Kakao ni zao kuu la biashara na linawaingiza fedha nyingi za kigeni. Tumekubaliana kuwa mawaziri wetu wa kilimo wakutane na waangalie ni maeneo gani ya kuweka mikataba ikiwemo utafutaji wa masoko na masuala ya utafiti,” alisema Waziri Mkuu Majaliwa ambaye alikuwa Abidjan kumwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika jukwaa la siku mbili la Maafisa Watendaji Wakuu barani Afrika lililomalizika jana.

Alisema mazungumzo yao yamefungua milango ya kuimarisha biashara na wamekubaliana na mwenyeji wake kwamba mawaziri wa nchi hizo wa viwanda na biashara pamoja na wa mambo ya nje wakutane na kuweka ajenda ya kwanza ya kufanyika kwa Jukwaa la Kibiashara baina ya Tanzania na Côte d’Ivoire.

“Tumekubaliana kuwa jukwaa hilo lifanyike mapema ili wafanyabiashara wetu wakutane na kubadilishana mbinu na hapa tunataka sekta binafsi ilisimamie eneo hilo. “Kupitia TPSF, taasisi zikae pamoja na kuainisha ni maeneo yapi ya kujengeana uwezo, iwe ni teknolojia mpya au ubadilishanaji wa wawekezaji katika mazao ya kokoa na korosho.”

“Tumewahakikishia kuwa tumepunguza muda wa kupata leseni nchini, tumeongeza maeneo ya uwekezaji (EPZA) na hivi karibu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button