Mange Kimambi Amtumia Ujumbe Trump Kuhusu Tanzania.
Mange Kimambi Amtumia Ujumbe Trump Kuhusu Tanzania.
Mange Kimambi amemuandikia barua Rais wa Marekani, Donald Trump, akimueleza kwamba akaunti zake za Meta-ikiwemo Instagram, ukurasa wa habari anaouendesha, na namba yake ya WhatsApp-zimefungwa baada ya kuzitumia kufichua ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu nchini Tanzania, huku akihimiza maandamano ya amani.
Kwenye barua hiyo, amefafanua kuwa wakati wa uchaguzi wa Oktoba 29, 2025, maandamano yaliyoongozwa na vijana wa Gen Z yalijibiwa kwa nguvu hatarishi za dola zilizoua watu, hali iliyolaaniwa na taasisi mbalimbali za kimataifa, na anasisitiza kuwa hatua ya Meta imeinyamazisha moja ya njia chache salama zilizobaki kwa Watanzania kupata taarifa za kweli.
Mange amemuomba Rais Trump kuihimiza Meta kurejesha akaunti zake, kuunga mkono sheria zitakazohakikisha uwazi na haki katika hatua za kuondoa akaunti za mitandao ya kijamii, na kushughulikia suala pana la majukwaa haya kudaiwa kushinikizwa na serikali ya Tanzania kukandamiza sauti za upinzani, akisema kuwa hatua hizo zinahatarisha ushiriki wa kidemokrasia na haki za binadamu.






