Rapper Megan thee stallion Rasmi amemwaga wino katika record label ya Warnermusic
Rapper wa kike kutokea nchini marekani Megan thee stallion rasmi amemwaga wino katika record label ya warnermusic ya Len Blavatnik huku akiwa ametoka kwenye label ya “1501 Certified Entertainment” aliyoondoka kwa madai ya kutoelewana na kuwekewa vikwazo vingi ikiwemo kutoa idadi chache ya nyimbo kwa muda mrefu.💔
Lakini pia Megan alifungua kesi akisaidiwa na Roc nation kuishtaki 1501 kuwa imeshikilia pesa zake za mirabaha kwa muda mrefu bila kumpa huku 1501 ikidai kuwa wanamdai Megan pesa za tour.
megantheestallion amekwisha jiunga na Warner Music Group na hii ni baada ya kukaa muda mrefu akiwa kama msanii huru.
Kampuni ya Warner Music Group inafahamika kwa ukubwa wake wa kulifikia soko duniani pamoja connection kwenye vituo vya redio na televisheni. duniani.💽🔥
Written By ✍️ @lilckey








