UZINDUZI WA MKAKATI WA KITAIFA WA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

UZINDUZI WA MKAKATI WA KITAIFA WA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amesema kuwa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia yatasaidia wanawake na vijana kupata muda mwingi wa kufanya kazi sambamba na kulinda afya zao.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo 08 Mei, 2024 amezindua Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ambapo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alishiriki.

Hafla hiyo imefanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam. Viongozi wengine walioshiriki hafla hiyo ni Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko, Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mhe. Dkt. Selemani Saidi Jafo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button