FBI, Polisi Marekani wajitosa nusu fainali Argentina na England

FBI, Polisi Marekani wajitosa nusu fainali Argentina na England

Mamlaka za usalama Marekani, FBI na Idara ya Polisi zimekutana na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kwa ajili ya kupanga mikakati ya kiusalama kwa mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Dunia baina ya Argentina na England utakaochezwa kesho Jumatano, Julai 15, 2026 saa 5:00 usiku kwa muda wa Afrika Mashariki.

Mechi hiyo inatazamwa kama yenye tishio kubwa zaidi la kiusalama kwa mashabiki na watu binafsi kutokana na uhasama uliopo baina ya timu hizo mbili.

Sababu kubwa inayotajwa kuchochea uhasama baina ya timu hizo ni ugomvi wa kuwania visiwa vya Falklands kati ya mataifa ya England na Argentina.

Chanzo cha uhasama huo wa kihistoria ni vita ya Falklands iliyopiganwa mwaka 1982 kuwania visiwa hivyo vilivyo chini ya England kwa sasa huku Argentina ikiendelea kusisitiza kuwa ni mali yake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button